UCHUMI

Dar es Salaam. Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma(PPRA) imebaini ufisafi wa Sh13.48 bilioni katika miradi miwili ya ujenzi wa majengo ya Mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi(GEPF) na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) baada ya kufanya ukaguzi katika majengo hayo.
Kadhalika PPRA, imeagiza GEPF kurejesha kiasi cha Sh847 milioni kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutokana na udanganyifu kwa kuagiza vifaa kupitia msamaha wa kodi uliotolewa, ambapo vifaa hivyo havikutumika katika mradi huo kwa mujibu wa maelewano.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Matern Lumbanga alisema timu ya wataalamu iliyoundwa kufanya uhakiki kuhusu hoja zilizotolewa awali ambazo zilionyesha malipo yenye shaka yaliyofanywa na taasisi hizo.

No comments:

Post a Comment

AJALI YA MOTO SHULE YA OLD TANGA

Ajali ya moto yatokea shule ya sekondari old tanga leo tarehe 18/09/2019 mchana.kwa mujibu wa kamanda wa polisi chanzo cha ajali hiyo a...